Historia Kuu ya Afrika (kwa Kiingereza w: General History of Africa (GHA)) ni mradi wa UNESCO ulioanzishwa tangu mwaka 1964.
Shabaha ya mradi ni kusahihisha “maelezo mapotovu yaliyokuwa yakieleza umaskini na ushenzi katika bara hili” kwa “kufanya uchunguzi mwafaka wa habari usiokuwa na upendeleo” . Uliona Historia ya Afrika “imeharibiwa mno kutokana na kutokujua na ubinafsi wa watu walioiandika” [1] .
Awamu ya kwanza hadi mwaka 1999 ilikuwa kuandika na kutoa vitabu 8 kuhusu Historia Kuu ya Afrika.
Awamu ya pili tangu mwaka 2009 inalenga kuandaa muhtasari wa historia na vitabu pamoja na misaada kwa walimu wa shule.
© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search